Waliobakwa DRC wana machungu kiasi cha kushindwa kusimulia ili wasaidiwe
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC matukio ya ukatili wa kingono ikiwemo ubakaji yanaendelea kutekelezwa kimfumo na vikundi vinavyopigana kwenye taifa hilo lililoshuhudia mapigano mara kwa mara. Flora Nducha na ripoti kamili.
Mjini Bunia, jimboni Ituri nchini DR Congo, katika ofisi za shirika la kiraia la SOFEPADI, linalosaidia wanawake na watoto waliokumbwa na ukatili wa kingono na ubakaji.