Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

13 Septemba 2019

Katika jarida la kina leo hii Flora Nducha anakuletea

-Kenya imezindua rasmi chanjo ya kwanza ya malaria iliyo kwenye majaribio, ugonjwa ambao hukatili maisha ya maelfu ya watu kila mwaka.

-Shirika la elimu sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO limeonya kwamba hatua za haraka zisipochukuliwa watoto milioni 12 hawatowahi kuonja shule ifikapo 2030

Sauti
10'47"
Matthew Dakin

UNESCO yasema utamaduni na chakula ni chachu ya kutimiza SDGs

Kongamano la kimataifa lililoandaliwa na shirika la Umoja wa Mataoifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO limeanza leo mjini Parma Italia likimulika jinsi gani chakula na utamaduni vinavyoweza kutoa suluhu ya changamoto zinazoikabili dunia za ongezeko la idadi ya watu duniani, mabadiliko ya tabianchi na jukwaa kwa ajili ya majadiliano ya jamii jumuishi. 

Sauti
2'1"
UNifeed Video

Majadiliano ya kuunda serikali mpya Sudan Kusini yamefanyika kwa awamu ya pili mjini Juba

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir na aliyekuwa naibu wake Riek Machar wamekamilisha majadiliano ya siku ya pili mjini Juba nchini Sudan Kusini huku viongozi hao wawili wakirejelea azma ya kufikia amani huku wakiahidi kukutana mara kwa mara kuelekea uundaji wa serikali ya mpya ya umoja wa kitaifa inayotarajiwa Novemba 12 mwaka huu 2019.

Sauti
2'43"