Wakwepa kodi wanalindwa, wafichua taarifa wanashtakiwa- Mtaalamu
Wafichua taarifa ni mashujaa wa zama za sasa na wanatekeleza majukumu yao kwa maslahi ya jamii na haki za binadamu hivyo hawapaswi kushtakiwa kwa kutoa taarifa kuhusu ukwepaji kodi. #luxleaks
Hiyo ni kauli ya mtaalam huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu uendelezaji wa utaratibu wa kimataifa wa demokrasia na haki, Alfred de Zayas aliyotoa kufuatia ripoti za kuhukumiwa kwa waliotoa taarifa kuhusu sakata la Lux.