Sekta ya tumbaku tumia mitandao ya kijamii kwahitaji mpango wa kiamataifa:WHO
Matumizi ya tovuti kuchagiza uraibu kama wa sigara yametajwa kama moja ya changamoto kubwa katika juhudi za kimataifa za kupunguza uvutaji sigara wamesema wataalamu wa afya wa Umoja wa Mataifa Jumatatu.
Katika wito wa kuchukua hatua kabla ya mkutano wa kimataifa wa udhibiti wa bidhaa za tumbaku , shirika la afya duniani WHO limesema, nchi ni lazima zishirikiane kufuatilia matangazo hoyo kila pembe duniani.