Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Perina Nakang alenga kushinda Olimpiki kuinua timu na familia yake

Perina Nakang alenga kushinda Olimpiki kuinua timu na familia yake

Pakua

Perina Nakang, ni mmoja wa wanariadha 37 wanaounda timu thabiti ya wakimbizi kwenye michezo ya Olimpiki iliyoanza leo Julai 26 huko Paris, Ufaransa. Familia yake ilikimbia Sudan Kusini kwa sababu ya vita yeye akiwa na umri wa miaka 7 na kufika kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya. Sasa ana umri wa miaka 21, akikimbia mbio za mita 800 ambapo katika mazoezi alimaliza kwa muda wa dakika 2 na sekunde 12 na lengo lake ni kufikia muda wa dakika 2 na sekunde 10. Assumpta Massoi katika makala hii iliyoandaliwa na UNHCR anamulika safari yake ya mazoezi na ndoto yake Perina.

Audio Credit
Bosco Vincent/Assumpta Massoi
Sauti
3'41"
Photo Credit
© IOC/John Huet