Mashambulizi mashariki mwa DRC yafurusha watu 20,000
Mashambulizi dhidi ya raia huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC yamesababisha watu 20,000 kukimbia makazi yao licha ya hatua ya Rais Felix Tshisekedi ya kutangaza hali ya hatari katika majimbo ya Ituri na Kivu Kaskazini tarehe 6 mwezi Mei mwaka huu.