Skip to main content

Chuja:

#ADF

UNICEF VIDEO

Wanahabari watoto wapasha umma kuhusu changamoto za maji DRC kwa kuwezeshwa na UNICEF

Hii leo ni siku ya maji duniani na ninakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako huko mtoto Liesse mwenye umri wa miaka 17 amefuatilia upatikanaji wa maji safi ya kunywa kwenye eneo la Goma jimboni Kivu Kaskaizini baada ya kupatiwa mafunzo ya uandishi wa habari na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF na hatimaye taarifa yake kutangazwa na Radio Okapi ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo.

Sauti
2'23"

04 JUNI 2021

Katika jarida la mada kwa kina kutoka Umoja wa Mataifa hii leo Leah Mushi anakuletea:

-Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema mashambulizi makali yanayotekelezwa na wapiganaji wa kundi la Allied Democratic Forces ADF, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC yamewalazimisha takriban watu 5,800 kukimbia mara kadhaa katika makazi ya watu waliotawanywa katika jimbo la Ituri Mashariki mwa nchi hiyo

Sauti
12'19"

02 JUNI 2021

Hii leo jaridani Leah Mushi anaanzia huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako waasi wa ADF wameshambulia kambi za wakimbizi wa ndani na kuua raia 55, UN umetoa taarifa ya kulaani. Atasalia huko huko Maziwa Makuu akimulika wakimbizi waliongia nchini Rwanda wakikimbia volkano ya Nyiragongo huko DRC na kisha atamulika pia suala la ndoa za utotoni. Makala tunamkaribisha John Kibego kutoka Uganda na mashinani ni ujumbe kutoka UNAIDS, karibu!

© FAO-Magnum Photos/Alex Webb

Tutumie misimu ya matunda kila wakati ili kupata virutubisho kwa bei nafuu

Tukiwa bado katika mwaka wa mbogamboga na matunda, mtaalamu wa lishe ambaye pia ni Mkurugenzi wa shirika la lishe la Nutrition International Kenya, Bi. Martha Nyagaya anashauri watu wawe wanatumia misimu ya matunda kuhakikisha wanakula matunda ya misimu hiyo ili kuepuka gharama na kuepuka kula tunda moja tu kwa kipindi chote kwani matunda na mbogamboga tofautitofauti zina manufaa tofautitofauti mwilini. Kupitia mahojiano haya yaliyofanywa na mwandishi wetu wa Kenya Jason Nyakundi, Bi.

Sauti
3'27"