Katu hedhi isiwe mwiko, mnahatarisha afya ya wanawake na wasichana- Wataalamu
Wataalamu 7 wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wametoa wito kwa jamii ya kimataifa iondokane na mwiko unaozingira suala la afya ya hedhi na badala yake ichukue hatua kuhakikisha fikra baguzi dhidi ya suala hilo zinabadilishwa na afya ya hedhi kwa wanawake na wasichana inalindwa.