Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu António Guterres akitoa hotuba yake maalum kuhusu hatua za hali ya hewa kutoka katika Jumba la Makumbusho la Marekani la Historia ya Asili mjini New York.
United Nations

Lengo la kudhibiti ongezeko la joto duniani kwenye nyuzijoto 1.5 linaning’inia - Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres asubuhi ya leo saa za New York, Marekani kupitia Hotuba Maalumu kuhusu Hatua Dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi ametahadharisha kuhusu hatari ya wazi ya uwezekano wa ongezeko la joto juu ya nyuzijoto 1.5 za selsiasi linaloukabili ulimwengu ikiwa uzalishalishaji wa hewa chafuzi utaendelea kwa viwango vya sasa.

Sauti
2'7"
Chakula kinachohitajika sana kikisambazwa na WFP huko Cité Soleil, Haiti.
© WFP/Tanya Birkbeck

Licha ya hali tete ya usalama, WFP yafanikiwa kufikisha Msaada wa chakula nchini Haiti

Licha ya machafuko na mashambulizi yanayofanywa na makundi yenye silaha huko nchini Haiti, shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani limeendelea kuimarisha operesheni zake katika mji mkuu wa Port-au-Prince na kusaidia jamii zilizoathiriwa na ghasia ambapo kwa mwezi Mei shirika hilo limeweza kuwafikia zaidi ya watu 93,000.

Sauti
3'23"