Takriban watu mil 33 wanahitaji msaada wa kuokoa maisha katika Ukanda wa Sahel
Maisha ya watu milioni 32.8 katika eneo zima la Ukanda wa Sahel wameathiriwa na mchanganyiko wa majanga mbalimbali ambayo yanazidisha ukosefu wa utulivu na kuzorotesha hali ya usalama na athari za mabadiliko ya tabianchi na kuwafanya watu wengi kuwa tegemezi wa msaada wa kibinadamu na huduma za ulinzi.