‘Tamu chungu’ kwa watu wa asili zawekwa bayana kwenye IW2024
Mkutano wa 23 wa Jukwaa la Kudumu kuhusu Masuala ya Watu wa Asili, UNPFII likiwa leo limeingia siku ya nne kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani, miongoni mwa mambo yaliyofanyika ni uzinduzi wa kitabu cha mwaka huu wa 2024 kuhusu watu wa asili kikipatiwa jina Dunia ya Watu wa asili, au IW2024, kikiwa ni toleo la 38.