Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mzozo nchini Sudan umewakosesha makazi maelfu ya watoto na familia zao.
© UNICEF/Ahmed Elfatih Mohamdee

Sasa ni dola bilioni 1 zinahitajika kusaidia mamilioni wanaokimbia mzozo wa Sudan - UNHCR

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), na mashirika 64 ya kibinadamu na kiraia leo Septemba 04 yametoa wito wa dola bilioni 1 kutoa msaada muhimu na ulinzi kwa zaidi ya watu milioni 1.8 wa Sudan wanaotarajiwa kuwasili katika nchi tano jirani ifikapo mwisho wa 2023, wakikimbia vita vinavyoendelea nchini mwao Sudan.

Mchoro wenye ujumbe nchini DRC
UN/Esther Nsapu

Mauaji ya watu 43 Goma, OHCHR yatoa tamko

Ofisi ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu, (OHCHR) imesema imekumbwa na hofu kubwa juu ya taarifa za vifo vya watu takribani 43 huko Goma, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, vifo vilivyotokea wakati wa maandamano dhidi ya Umoja wa Mataifa na mashirika mengine siku ya Jumatano ambako pia watu 56 walijeruhiwa.

Soka kwa ajili ya malengo ya maendeleo endelevu.
UNSOM

Kenya: Global Youth Forum  na UNIS Nairobi watekeleza mradi wa ‘Football for the Goals’ kwa vitendo

Peter Omondi kutoka shirika la vijana la Global Youth Forum nchini Kenya ni mmoja wa vijana ambao mapema mwezi huu kwa kushirikiana na Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa, UNIS Nairobi waliandaa mechi ya mpira wa miguu iliyohusisha zaidi ya vijana 100 katika Kaunti ya Siaya ili kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu.

Sauti
2'41"