Sasa ni dola bilioni 1 zinahitajika kusaidia mamilioni wanaokimbia mzozo wa Sudan - UNHCR
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), na mashirika 64 ya kibinadamu na kiraia leo Septemba 04 yametoa wito wa dola bilioni 1 kutoa msaada muhimu na ulinzi kwa zaidi ya watu milioni 1.8 wa Sudan wanaotarajiwa kuwasili katika nchi tano jirani ifikapo mwisho wa 2023, wakikimbia vita vinavyoendelea nchini mwao Sudan.