Viongozi wa dunia wanakutana UN; Ni kupima ‘mapigo ya moyo’ wa dunia
Wakati ule umewadia tena! Macho na masikio ya dunia kuelekezwa makao makuu ya UN jijini New York, Marekani baadaye mwezi huu wakati Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, (UNGA) litakapokaribisha marais, malkia na wafalme, mawaziri wakuu na wakuu wa nchi kutoka nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa.