Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Rais Joe Biden wa Marekani akihutubia Mjadala Mkuu wa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani 19 Septemba 2023.
UN /Cia Pak

Idhinisheni ujumbe wa kuimarisha usalama Haiti; Biden aliambia Baraza la Usalama UN

Kuunga mkono utayari wa Kenya kuongoza ujumbe wa kipolisi unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa nchini Haiti na suala la nafasi ya umoja katika kukabili changamoto zinazokabili dunia hivi sasa ni miongoni mwa mambo aliyogusia Rais wa Marekani Joe Biden wakati akihutubia siku ya kwanza ya Mjadala Mkuu wa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.

Wasichana wa baraza la ushauri la vijana, Nairobi wakitazama app ya OKY.
UNICEF Kenya

Apu ya OKY na hedhi salama yasongesha SDG 3- UNICEF

Shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, limezindua apu maalum ya wasichana kufuatilia maelezo wakati wa hedhi. Apu hiyo ni mahsusi kwa wasichana wa mataifa yanayoinukia na yaliyo masikini. Apu hii inaleta matumaini wakati huu ambapo viongozi wa dunia wanakutana New York, Marekani kutathmini maendeleo ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. 

Sauti
2'47"
Csaba Kőrösi (kushoto) Rais wa mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la UN akikabishi rungu la kuongoza mkutano kwa Rais wa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la UN (UNGA78). Kulia kabisa ni Naibu Katibu Mkuu wa UN Amina J. Mohammed
UN /Manuel Elias

UNGA 77 yafunga pazia, Rais wa UNGA78 ala kiapo

Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umekunja jamvi asubuhi ya tarehe 5 Septemba 2023, jijini New York, Marekani kwa Rais wa mkutano huo anayemaliza muda wake Csaba Kőrösi akisisitiza kuwa licha ya mikingamo ya kijiografia, ushirikiano baina ya nchi haukwepeki.