Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Inakadiriwa kuwa watoto milioni moja hawako shuleni nchini Haiti kutokana na ukosefu wa usalama na sababu nyingine.
© UNICEF

Ghasia za kutumia silaha dhidi ya shule zimeongezeka mara tisa Haiti katika mwaka mmoja: UNICEF

Vitendo vya unyanyasaji wa kutumia silaha dhidi ya shule nchini Haiti, vikiwemo vya risasi, uporaji, unyang’anyi na utekaji nyara vimeongezeka mara tisa katika kipindi cha mwaka mmoja, huku ongezeko la ukosefu wa usalama na machafuko makubwa vikianza kulemaza mfumo wa elimu nchini humo, limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF katika taarifa yake iliyotolewa mjini Pout-au-Prince na New York huku likiongeza kuwa watoto walipoteza wastani wa siku moja na nusu ya shule kwa wiki katika mwezi Januari mwaka huu 

Msichana akinywa maji katika  bustani wa shule yake huko Goré, kusini mwa Chad.
© UNICEF/Frank Dejongh

UNESCO: Mafanikio ya elimu yanatatizwa na ukosefu wa uwekezaji katika afya na lishe

Wakati kuwekeza katika afya na lishe shuleni kuna athari chanya kwa ufaulu wa watoto kitaaluma, shule 1 kati ya 3 duniani bado haina maji ya kunywa na vifaa vya msingi vya usafi wa mazingira, kulingana na ripoti mpya iliyozinduliwa leo 8 Februari na mashirika ya Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO, la kuhudumia watoto UNICEF, na la mpango wa chakula duniani WFP.