Mwanamke 1 anakufa kila baada ya dakika 2 kutokana na ujauzito- UN
Ni ajabu na kweli kwamba uzoefu unaotakiwa wa matumaini na chanya umegeuka kuwa shubiri na machungu kwa wanawake wajawazito amesema Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus baada ya ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa kufichua hii leo ya kwamba kila baada ya dakika 2 mwanamke mmoja anakufa kutokana na ujauzito au wakati anajifungua mtoto.