Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa UN anataoa wito wa ushirika wa amani duniani
Unsplash/Priscilla du Preez

Hebu tujenge ushirika wa amani, asema Katibu Mkuu wa UN

Hebu na tuazimie tena kujenga ushirika wa amani, ni sehemu ya ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliotoa hii leo ambao ni siku ya kimataifa ya udugu wa kibinadamu duniani, akisema wito wake huo unazingatia ongezeko la kauli za chuki, mizozo na misimamo mikali kwa misingi ya kiitikadi za kidini na makundi mbalimbali.

Mkulima akianika majani ya kunde kwa ajili ya matumizi ya baadae
FAO

Mkutano wa UN wa kutathmini mifumo ya uzalishaji chakula duniani kufanyika Italia mwezi Julai

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J.Mohammed amesema ana matarajio makubwa kwa Italia ambayo itakuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa kutathmini maendeleo  ya marekebisho  ya mifumo ya uzalishaji wa chakula duniani utakaofanyika mwezi Julai mwaka huu kwenye makao makuu ya shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO jijini Roma nchini Italia.

Mtoto akitabasamu darasani wakati wa ziara ya pamoja ya ECW na Norway kwenye maeneo nufaika ya miradi ya elimu inayofadhiliwa na pande mbili hizo.
ECW

Watoto milioni 222 walio katika maeneo yaliyoathirika na migogoro wanahitaji msaada wa haraka wa elimu:ECW 

Mfuko wa Umoja wa Mataifa unaohusika na kusongesha elimu kwenye maeneo yenye majanga na mizozo ya muda mrefu, Education Cannot Wait, ECW au kwa lugha ya Kiswahili, Elimu Haiwezi Kusubiri, pamoja na wadau wamesisitiza umuhimu wa kusaidia mamilioni ya watoto walio katika mazingira ya migogoro ili waweze kupata elimu, wakisema elimu ndio ufunguo wa kuwakomboa watoto hao hususan wasichana katika maisha yao ya siku za usoni.

Sauti
3'7"
Ben Lyimo, mwanafunzi wa mwaka wa pili kwenye Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo nchini Tanzania akilisha magugu maji aina ya Azolla kwa ng'ombe mkoani Morogoro, mashariki mwa Tanzania.
UN News

Azolla, gugu maji liligeuka mkombozi kwa wakulima, wafugaji na vijana Tanzania

Azolla ambao ni mmea aina ya magugu maji, umeanza kupata umaarufu duniani kutokana na uzalishaji wake wa kasi, ukitumia eneo dogo, halikadhali kwa kuwa ni lishe bora kwa mifugo kama vile ng’ombe na kuku.

Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO linasema Azolla ina kiwango kikubwa cha protini ghafi kuanzia asilimia 19 hadi 30, ikilinganishwa na mazao mengi ya kijani kibichi pamoja na yale yameayo kwenye maji.