Hebu tujenge ushirika wa amani, asema Katibu Mkuu wa UN
Hebu na tuazimie tena kujenga ushirika wa amani, ni sehemu ya ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliotoa hii leo ambao ni siku ya kimataifa ya udugu wa kibinadamu duniani, akisema wito wake huo unazingatia ongezeko la kauli za chuki, mizozo na misimamo mikali kwa misingi ya kiitikadi za kidini na makundi mbalimbali.