Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Geti la kuingia kwenye makao makuu ya ofisi ya haki za binadamu OHCHR mjini Geneva Uswis
UN Photo/Jean-Marc Ferré

Uchunguzi huru na wa haki lazima ufanyike dhidi ya waliokufa Laas Canood: Turk

Kutoka Geneva nchini Uswisi Kamisha Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa , Volker Turk ametoa wito kwa mamlaka ya Somalia kuhakikisha uchunguzi huru unafanyika bila upendeleo kufuatia mauaji yaliyotokea baada ya mapigano makali kuanzia tarehe 5 mwezi huu wa Februari nchini humo kati ya vikosi vya usalama na wanajamii wa ukoo wa Laas Canood.

Furaha (12) akiwa amembeba mdogo wake Isaac mwenye umri wa miaka 3 waliunganishwa tena na mama yao Furaha (kushoto) baada ya kupotezana kwa zaidi ya wiki 2 kutokana na mapigano mashariki mwa DRC.
© UNICEF/Jospin Benekire

UNICEF na wadau na mbinu ya kusaidia wazazi kuungana na watoto wao DRC

Makumi kwa mamia ya watoto wametenganishwa na familia zao katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC kutokana na mapigano makali yanayoendelea mashariki mwa nchi hiyo kati ya jeshi la serikali, FARDC na waasi wa M23. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kwa ushirikiano na shirika la kiraia la kuhudumia vijana na watoto walio katika mazingira magumu, CAJED, wamechukua hatua kuunganisha watoto na familia zao hatua iliyoleta furaha sio tu kwa walengwa lakini pia kwa jamii nzima.

Msichana mwenye umri wa miaka kumi alitoroka nyumbani baada ya kugundua familia yake ilipanga kumfunza kama ngariba wa ukeketaji/C. Kwa sasa anaishi katika nyumba salama ya UNICEF huko Port Loko, Sierra Leone, na anahudhuria shule.
© UNICEF/Olivier Asselin

Wanaume na wavulana jitokezeni mtokomeze FGM

Hii leo ni ikiwa ni siku ya kimataifa ya kutokomeza ukeketaji wa wanawake na wasichana ,Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaka wanaume na wavulana wapaze sauti zao kusaidia kutokomeza mila hiyo potofu na hatarishi.  

Sauti
2'10"