Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mkulima wa mwani visiwani Zanzibar nchini Tanzania
© FAO/S. Venturi

Mashirika ya UN yazindua mradi wa pamoja wa dola milioni 5 ili kuharakisha uwezeshaji wanawake Tanzania

Hii leo Jumatano visiwani Zanzibar nchini Tanzania, mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo la Chakula na Kilimo (FAO), Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) na kushughulikia masuala ya wanawake, (UN Women) wamezindua programu ya miaka mitano ya kuongeza kasi ya Uwezeshaji wa mradi wa uimarishaji uchumi wa wanawake wa Vijijini. 

Sauti
4'11"
Uchafuzi wa hewa katika mji wa Ulaanbaatar, Mongolia.
© UNICEF/Tamir Bayarsaikhan

Lazima tuongeze nishati mbadala mara mbili ya sasa katika miaka 8 ijayo: WMO

Shirika la Umoja wa Mataifa la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO limesema usambazaji wa umeme kutoka vyanzo vya nishati safi lazima uongezeke mara mbili ndani ya miaka minane ijayo ili kupunguza ongezeko la joto duniani na iwapo hilo halitafanyika, kuna hatari kwamba mabadiliko ya tabianchi, kuongezeka kwa hali mbaya zaidi ya hewa pamoja na shida ya maji vitadhoofisha uhakika wa upatikanaji wa nishati na hata kuhatarisha usambazaji wa nishati mbadala. 

Tukio la hali ya juu kuhusu,hukumu ya kifo.
UN Photo

Kuna uhusiano baina ya hukumu ya kifo, utesaji na ukatili mwingine: Wataalam UN 

Katika maadhimiosho ya 20 ya siku ya kupinga hukumu ya kifo duniani hii leo, wataalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu utesaji na ukatiuli mwingine , vitendo visivyo vya kibinadamu au vitendo vya udhalilishaji na adhabu Alice Edward, na yule wa kupinga mauaji ya kiholela, Morris Tidball-Binz wametoa taarifa ya pamoja inayotathimini uhusiano baina ya hukumu ya kifo na kupinga kabisa mateso na adhabu nyingine za kikatili, za kinyama au za kudhalilisha.