Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mtoto akipatiwa chanjo dhidi ya polio huko Cotonou nchini Benin
©Yézaël Adoukonou/ Nations Unies Bénin

COVID-19 yarudisha nyuma utoaji chanjo kwa watoto kwa miongo mitatu

Licha ya mwaka 2021 kutegemewa utakuwa mwaka bora wa utoaji chanjo kwa watoto wachanga baada ya janga la COVID-19 kuvuruga utoaji chanjo mwaka 2019 na 2020, ripoti iliyotolewa leo na Umoja wa Mataifa imeonyesha kiwango cha utoaji chanjo duniani kimeendelea kupungua maradufu na kurudisha takwimu kwa miongo mitatu nyuma huku watoto milioni 25 wakikosa chanjo muhimu za kuokoa maisha yao.

Sauti
2'51"
Spika Janja, spika ya kwanza kabisa janja kutengenezwa barani Afrika
Smart Kaya

Biashara ya huduma kuondoa Afrika kwenye utegemezi wa kilimo na madini- UNCTAD

Eneo la biashara huru barani Afrika linakua, idadi ya watu wenye kipato cha kati inaongezeka, halikadhalika soko la walaji linaibuka sambamba na huduma za kifedha na teknolojia, imesema Kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo, UNCTAD hii leo huku ikitanabaisha kuwa mambo yote hayo ni fursa kubwa kwa Afrika kupanua vyanzo vyake vya kujipatia kipato.

 

Charline (kushoto) mwenye umri wa miaka 11 amekimbia mapigano huko Bunagana jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC na kukimbilia eneo la Rutshuru yeye na familia yake. (Maktaba)
©UNICEF/Jean-Claude Wenga

Mapigano nchini DRC yanaathiri raia :UNHCR

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limeendelea kutoa wito wa sitisho la mashambulizi dhidi ya raia jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako matukio hayo yameendelea kusababisha vifo miongoni mwa raia. 

Kinu cha kuhifadhi nafaka huko Lvivska nchini Ukraine
© FAO/Viktoriia Mykhalchuk

Janga la chakula duniani: Mwale wa matumaini waonekana – Guterres

Hii leo huko Istanbul Uturuki tumeshuhudia hatua muhimu ya kuhakikisha kuwa mazao ya chakula zikiwemo nafaka kutoka Ukraine yanasafirishwa na kuuzwa nje ya nchi hiyo kwa usalama kupitia Bahari Nyeusi, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani baada ya makubaliano ya kuwezesha hatua hiyo iliyochukua muda mrefu kufikiwa.