Wavukao Mediteranea wapungua lakini vifo vyaongezeka- UNHCR
Ingawa idadi ya wakimbizi na wahamiaji wanaovuka bahari ya Mediteranea kwenda Ulaya imepungua, idadi ya wanaokufa imeongezeka, kwa kuwa safari ni za hatari zaidi, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR.