Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Tarehe 24 Aprili 2017, mtoto akipatiwa chanjo dhidi ya surua huko kambini Beerta Muuri mjini Baidoa nchini Somalia.
UNICEF/Yasin Mohamed Hersi

Kuna dalili za ‘kimbunga’ cha mlipuko wa Surua: WHO/UNICEF

Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa, lile la kuhudumia watoto, UNICEF na la afya duniani, WHO yamesema idadi ya wagonjwa wa surau duniani kwa miezi miwili ya mwanzo ya mwaka huu wa 2022 imeongezeka kwa asilimia 79 kulinganisha na kipindi kama hicho mwaka jana na hivyo kuwa ni mazingira yanayoweza kuchochea mlipuko wa ugonjwa huo unaozulika kwa chanjo.

Vital Bambanze (kulia) mwakilishi wa jamii ya watwa nchini Burundi akiwa kwenye majadiliano na washiriki wengine wakati wa mkutano wa 21 wa jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la watu wa asili, UNPFII mwezi Aprili 2022 jijini New York, Marekani.
UN/ Flora Nducha

Nuru Burundi kwa haki za jamii ya Watwa

Mkutano wa 21 wa Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la watu wa asili, UNPFFII likiwa limeingia siku ya tatu kwenye makao makuu ya Umoja huo jijini New York, Marekani, washiriki kutoka Burundi wameieleza Idhaa ya Kiswahili ya  Umoja wa Mataifa juu ya hatua zinazoendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha haki za binadamu za jamii ya asili aina ya watwa zinazingatiwa.

 

UN Ethiopia/Getachew Dibaba
Takriban mifugo milioni moja wamekufa kutokana na ukame katika eneo la Somali nchini Ethiopia.

Huu ni ukame mbaya zaidi kuwahi kutokea kwa miaka 40, Mamilioni ya Waethiopia hatarini:UN

Jimbo la Somali lilioko Mashariki mwa Ethiopia limekumbwa na misimu mitatu ya kiwango kidogo cha mvua kilicho chini ya wastani, hali ambayo inazidisha madhila  ya kibinadamu kwa watu wapatao milioni 3.5, ambao ni zaidi ya nusu ya wakazi wa eneo hilo ambao tayari walikuwa katika shida.