Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wakimbizi huko Minawao, kaskazini mashariki mwa Kamerun, wanapanda miti katika mkoa ambao umekatwa misitu kwa sababu ya mabadiliko ya hali ya hewa na shughuli za kibinadamu.
© UNHCR/Xavier Bourgois

Mradi wa upandaji miti wanufaisha wakimbizi nchini Cameroon

Mradi kabambe wa upandaji miti, ulioanzishwa mwaka 2018 katika kambi ya wakimbizi ya Minawao nchini Cameroon kwa ushirikiano kati ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi duniani, UNHCR na shirikisho la waluteri duniani, LWF umesaidia kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi na kuzuia kuenea kwa jangwa katika ukanda wa Sahel. Leah Mushi ana taarifa zaidi kutoka katika video ya UNHCR.

Sauti
1'40"
Wakulima wakilisha mifugo Ethiopia.
FAO/IFAD/WFP/Petterik Wiggers

Mradi wa IFAD umeongeza siyo tu milo bora bali pia kipato- Wakulima Ethiopia

Mkutano wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa umefanyika hii leo jiijni New York, Marekani kando mwa mjadala mkuu wa mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA76 ambapo vioingozi wa nchi 193 wa Umoja huo wamejadili mifumo endelevu ya chakula ya kuwezesha wakulima kulima mazao bila vikwazo na vile vile kuzalisha vyakula vyenye lishe sambamba na kuongeza kipato.

 

Sauti
1'39"