Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa akisafisha mikono kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, New York.
UN Photo/Loey Felipe

COVID-19: Idadi ya wanaoingia jengo la UN New York yapunguzwa kwa asilimia 60 wakiwemo wafanyakazi

Wakati maambukizi mapya ya virusi vya Corona au COVID-19 yakiendelea kuongezeka katika nchi nyingi duniani na idadi ya waliofariki kutokana na virusi hivyo ikiongezeka kila uchao, Umoja wa Mataifa nao umechukua hatua kudhibiti maambukizi kwa kupunguza idadi ya wafanyakazi wanaofika kazini kila siku kwa asilimia 60. Hii ni kwa kuzingatia kuwa tayari visa vimeripotiwa katika miji kadhaa ikiwemo New York, Marekani ambako ndiko makao makuu ya chombo hicho.

Sauti
2'36"