Kubebwa muda mrefu, kuendeshwa kwenye vigari na kutumia skrini muda mwingi kwadumaza watoto- WHO
Mwongozo mpya wa shirika la afya ulimwenguni, WHO unatoa maelekezo ya jinsi ambavyo watoto wenye umri wa chini ya miaka 5 wanatakiwa kucheza na kufanya shughuli zinazohusisha maungo yao badala ya kubebwa wakati wote au kutumia muda mwingi kwenye skrini za televisheni au michezo yao.