Tusipomakinika Jodari watatoweka: UN
Samaki Jodari au maarufu kama Tuna ni samaki wanaopendwa kwa sababu mbalimbali, kuanzia kutoa lishe bora hata kutumiwa katika kuburudisha mashuleni, lakini sasa wako katika hatari kubwa ya kutokuwa endelevu na kuweka mustakhbali wao njia panda umesema leo Umoja wa Mataifa.