Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Uhaba wa chakula kukumba nchi za kusini mwa Afrika

Mashirika ya Umoja wa Mataifa ikiwemo lile la mpango wa chakula, WFP na lile la chakula na kilimo FAO na ofisi ya usaidizi wa dharura, OCHA yamesema kwamba ukosefu wa nvua mwishoni mwa mwaka 2017 na mwanzoni mwa mwaka huu wa 2018 unahatarisha uzalishaji wa chakula kwa nchi za kusini mwa Afrika.

Kutoka ngariba hadi mkunga

Nchini Djibouti, ngariba aliyekuwa akitumia mikono yake kukeketa watoto wa kike na wanawake, FGM sasa anatumia mikono hiyo kusaidia wanawake wajifungue salama. Ngariba huyo Fatouma Ali baada ya kubadilika amesaidia kuepusha watoto wa kike zaidi ya 200 wasikumbwa na ukeketaji.