Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tochi ya Olimpiki iangazie mshikamano wa amani kimataifa:Guterres 

Nembo ya olimpiki ikiwa na miduara mitano ikimaanisha idadi ya mabara ambayo yanashikiri michuano hiyo.
UN/Eskinder Debebe
Nembo ya olimpiki ikiwa na miduara mitano ikimaanisha idadi ya mabara ambayo yanashikiri michuano hiyo.

Tochi ya Olimpiki iangazie mshikamano wa amani kimataifa:Guterres 

Utamaduni na Elimu

Juma hili maelfu ya watu na hususani wanamichezo wanakusanyika mjini PyeongChang huko Jamhuri ya Korea, kwa ni ya kushiriki mashindano ya Olimpiki ambayo ni ya kirafiki, yenye mshikamano, na ya kuheshimiana.

Katika ujumbe wake maalumu kwa ajili ya michezo hiyo ya Olimpiki inayojumuisha pia Olimpiki ya walemavu  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema hushirikisha wanariadha bora duniani na kwamba mashindayo hayo yaliyoanza katika enzi za Ugiriki ya kale, yanatoa nafasi kwa washiriki wanariadha na watazamaji, kusafiri kwa amani na pia kudumisha amani  miongoni mwa washiriki  wakati wote michezo inapofanyika. 

Na kwa mantiki hiyo amesema “jamii yetu inaweza kuvuka tofauti zote za kisiasa”.  Akiongeza kuwa inaenda sanjari na wakati wa sasa hasa katika rasi ya Korea, akitoa wito kwa pande zote husika katika mgogoro wa rasi hiyo kuheshimu dhamira ya olimpiki wakati wa  michezo ya 2018 ya olimpiki ya kawaida na ile ya walemavu.

Bendera za Umoja wa Mataifa na ile ya Olimpiki zikiwa zinapepea kwa pamoja kwenye makao makuu ya umoja huo kabla ya kuwashwa kwa mwenge wa olimpiki
UN/Eskinder Debebe
Bendera za Umoja wa Mataifa na ile ya Olimpiki zikiwa zinapepea kwa pamoja kwenye makao makuu ya umoja huo kabla ya kuwashwa kwa mwenge wa olimpiki
Bendera za Umoja wa Mataifa na ile ya Olimpiki zikiwa zinapepea kwa pamoja kwenye makao makuu ya umoja huo kabla ya kuwashwa kwa mwenge wa olimpiki, by UN/Eskinder Debebe

Amechagiza na hebu mwanga wa Olimpiki umulike kama ishara  ya mshikamano wa binadamu wote, na dhamira ya Olimpiki isaidie kusambaza utamaduni wa amani.

Naye mwanariadha nyota mkimbizi wa Sudan kusini, Yiech Pur Biel ambaye tayari yuko PyeongChang kwa ajili ya mashindano hayo amebeba ujumbe maalumu kwamba “Amani ni msingi wa kila kitu ambacho serikali inaweza kufanya, na kila hatua kuelekea amani ni muhimu”.

Pur Biel alilazimika kukimbia machafuko Sudan Kusini mwaka 2005 akiwa na umri wa miaka 10 tu akiwaacha nyuma wazazi wake na kwenda kuishi kambi ya Kakuma nchini Kenya.

Amesema amehamasishwa kwamba wawakilishi wa Korea ya Kaskazini (DPRK) na Jamhuri ya Korea Kusini watatembea pamoja wakipeperusha bendera ya Olimpiki katika mashindano hayo yatakayoanza rasmi kesho Februari 9.