KM ametangaza kumteua raia wa Mali kuwa Mshauri Maalumu kwa Afrika
Cheikh Sidi Diarra wa Mali ameteuliwa na KM Ban Ki-moon kuwa Mshauri mpya Maalumu kuhusu Masuala ya Afrika, na pia kuchukua wadhifa wa Mwakilishi Mkuu wa Nchi Masikini, Nchi Zisio Bandari pamoja na Nchi za Visiwa Vidogo Vidogo.