Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiwa na washiriki wengine wa tukio la Kwibuka30 wakiwasha mishumaa kukumbuka waliopoteza maisha wakati wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda yaliyofanyika kwa siku 100 kuanzia Aprili 7, 1994
UN /Eskinder Debebe

Kwibuka30: Vijana kemeeni kauli za chuki kokote muisikiapo na muionapo – Guterres

Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, Baraza Kuu limekuwa na tukio maalum la kumbukizi ya miaka 30 ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda au KWIBUKA30, ambapo Katibu Mkuu wa Umoja huo, Antonio Guterres ametumia hotuba yake pamoja na mambo mengine kuwasihi vijana kutoka taifa hilo la Afrika Mashariki kukemea chuki kokote wanapoisikia au kuiona. 

Mvulana anakimbia katika mitaa iliyoharibiwa ya Gaza.
© UNRWA/Ashraf Amra

GAZA: Miezi 6 ya mzozo Guterres akemea matumizi ya Akili Mnemba

Kesho kutwa jumapili ikiwa ndio itatimu miezi sita ya mzozo wa Gaza, huko Mashariki ya Kati, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo amezungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani akirejelea wito wake wa sitisho la mapigano kwa misinigi ya kiutu, kuachiliwa kwa mateka wote bila masharti, ulinzi wa raia na misaada ya kiutu ifikie walengwa bila vikwazo vyovyote huku akikgusia pia Israeli kutumia akili mnemba kwenye operesheni zake. 

Audio Duration
2'40"
Ufunguzi wa kituo cha malezi ya watoto wachanga huko Kajiado nchini Kenya ili kuwezesha mama zao kurudi shule.
UN News

Wadau nchini Kenya waitikia wito wa Umoja wa Mataifa wa kumwezesha mtoto wa kike

Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ulifunga pazia hivi majuzi jijini New York Marekani ukipigia chepuo uwekezaji kwa wanawake na wasichana, na leo tunabisha hodi nchini Kenya wasichana waliokumbwa na ujauzito utotoni na kukatishwa ndoto za kuendelea na masomo au kupata ajira wamepata jawabu la changamoto wanazokumbana nazo pindi wakijifungua watoto wao. 

Sauti
7'35"