Soma Bag: Mabegi ya mgongoni yanayotumia sola mkombozi kwa wanafunzi
Lengo namba nne la Malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa SDGs linazungumzia juu ya elimu bora, yenye usawa na kutoa fursa kwa wote, na hicho ndicho kinachofanyika jijini Mwanza kaskazini Magharibi mwa Tanzania ambapo vijana wamebuni mradi wa mabegi yanayokusanya nishati ya jua ili kuwasaidia wanafunzi waishio vijijini kujisomea nyakati za usiku.