Haki ya kutafuta hifadhi ni haki ya msingi ya kibinadamu: Guterres
Wakati duniani inaadhimisha siku ya wakimbizi duniani hii leo kwa kuwa na idadi kubwa kabisa ya wakimbizi kuwahi kurekodiwa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anasema siku hii itumike kutafakari juu ya ujasiri wa wale wanaokimbia vita, vurugu na mateso pamoja na kutambua huruma ya wale wanaowakaribisha wakimbizi hao.