Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Watoto wa Darfur Kaskazini kambi ya wakimbizi wa ndani ya Abo Shouk ambako UNAMID imekarabati darasa.
UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Vita, Machafuko na majanga mengine vyatawanya watoto milioni 36.5 mwaka 2021: UNICEF 

Vita, machafuko na mjanga mengine vimewaacha watoto milioni 36.5 wakitawanywa kutoka majumbani kwao hadi kufikia mwisho wa mwaka 2021 kwa mujibu wa takwimu mpya zilizotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF ambalo linasema idadi hiyo ni kubwa kabisa kurekodiwa tangu vita ya pili ya dunia.

Sauti
3'36"
Emma Theofelus ambaye ni Naibu Waziri wa Habari wa sasa nchini Namibia na mshindi wa tuzo ya UNFPA.
UNFPA

Emma Theofelus wa Namibia na BKKBN ya Indonesia ndio washindi wa Tuzo ya UNFPA mwaka 2022 

Tuzo ya kila mwaka ya shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi, UNFPA ambayo hutolewa kwa mtu binafsi na shirika au taasisi inayojikita katika kuboresha afya ya uzazi kwa wanawake, pamoja na afya ya akina mama na wajawazito, mwaka huu imeenda kwa Emma Theofelus ambaye ni Naibu Waziri wa Habari wa sasa nchini Namibia na mshindi wa kwanza mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kupata tuzo hiyo.

Sauti
3'12"
Lucas na kaka yake wote wana  ualbino ambao unasababisha ngozi yao kupata matatizo na uoni wao ni hafifu.
UNICEF

Tuwajumuishe watu wenye ualbino kwenye mijadala:UN 

Ikiwa leo dunia inaadhimisha siku ya kimataifa ya kuelimisha jamii kuhusu watu wenye ualbino, Umoja wa Mataifa umetoa  rai kwa nchi zote duniani kuwajumuisha watu wenye ualbino katika mijadala na mipango inayoathiri haki zao za kibinadamu, ili kuhakikisha wanafurahia usawa na ulinzi unaotolewa kwao katika sheria na viwango vya kimataifa.

Sauti
2'24"
Uchunaji wa kahawa San Marcos nchini Guatemala.
Unsplash/Gerson Cifuentes

Sekta zote zihusishwe ili kuondoa tatizo la ajira za watoto Guatemala

Ikiwa leo wakuu wa nchi na wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani wanakutana katika mkutano wa 110 wa Kimataifa wa wanachama wa shirika hilo kujadili hatua za haraka zinazoweza kuchukuliwa ili kukabiliana na athari za ajira na kijamii za migogoro mingi iliyoibuka duniani nchini Guatemala wadau wamehimiza sekta zote kujumuishwa ili kutatua tatizo la ajira kwa watoto.

Sauti
2'12"
Ibrahim mtoto wa miezi 8 anayeugua utapiamlo akifanyiwa vipimo katika hospitali ya Moghadishu Somalia
© UNICEF/Omid Fazel

Ukiona watoto wenye utapiamlo pembe ya Afrika utalia 

Mwaka 2011 dunia ilitangaziwa kuwepo kwa baa la njaa nchini Somalia ambapo zaidi ya watoto laki 340,000 walikuwa na utapiamlo, na ingawa mwaka huu bado baa la njaa halijatangazwa rasmi nchini humo lakini Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema hali ni tete na watoto zaidi ya laki 380,000 wana utapiamlo mkali ambapo hata ukiwaona watoto hao machozi yatakutoka.

Sauti
2'31"