Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Jengo la dawati la jinsia na watoto kwa ajili ya kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia na mila kandamizi dhidi ya wanawake na wasichana
Picha: UNFPA/Warren Bright

UNFPA Tanzania yakabidhi msaada wa dawati la jinsia wilayani Simanjiro

Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani na masuala ya afya ya uzazi UNFPA nchini Tanzania limekabidhi jeshi la polisi mkoani Manyara msaada wa jengo la dawati la jinsia na watoto ikiwa njia moja wapo ya jitihada za kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia na mila kandamizi dhidi ya wanawake, wasichana na watoto.

Sauti
4'59"
Luteni Kanali Amin Stevin Mshana (katikati), Mkuu wa TANZBATT 6 akiwasili Berbérati, Mambéré-Kadéï, Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR.
TANZBATT 6/Kapteni Mwijage Inyoma

TANBAT 5 yakabidhi jukumu la ulinzi wa amani wa UN kwa TANBAT 6 nchini CAR

Kikosi cha 5 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, TANBAT 5 kilichokuwa kinahudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, MINUSCA, kimekamilisha muda wake  na kukipisha kikosi kingine cha 6 nacho kutoka Tanzania, TANBAT 6 ambacho kitaendeleza jukumu hilo. Kutoka Berberat, Kapteni Mwijage Inyoma ni Afisa Habari wa TANBAT 6 ametuandalia taarifa hii. 

Sauti
2'35"
Charlotte Fatuma, mkimbizi kutoka DRC anaendesha duka kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Coranne nchini Msumbiji kutokana na umeme ambao umefanikishwa na mradi unaotekelezwa na UNHCR, Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika.
UNHCR Video

Utu na maendeleo vyakutanishwa Coranne na kuleta ustawi kwa wakimbizi na wenyeji

Charlotte Fatuma na Neema Cenga ni wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na sasa wanaishi ukimbizini nchini Msumbiji katika jimbo la Nampula. Kwa sasa Charlotte ni mjasiriamali mwenye mafanikio makubwa, akiendesha biashara ya duka kwenye makazi ya wakimbizi ya Coranne huku Neema naye akijitahidi kulea na kusomesha watoto wake.  

Sauti
4'28"
Maelfu ya familia wamehama makazi yao kutokana na ukame wa hivi karibuni nchini Ethiopia
© UNHCR/Eugene Sibomana

Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza atembelea waathirika wa ukame Ethiopia atoa ahadi ya kuendelea ushirikiano na UN

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, James Cleverly akiambatana na Mwakilishi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Ethiopia, Gianfranco Rotigliano wametembelea eneo la Afar, nchini Ethiopia kujionea athari za ukame kwa watoto na familia na kutathimini hatua za dharura zizazochukuliwa na UNICEF ambapo Uingereza ni mdau muhimu kama mwanachama wa Umoja wa Mataifa na muhisani.

Sauti
2'12"