Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Walinda amani kutoka Tanzania na Indonesia wakikagua daraja.
TANZBATT 7/Ibrahim Mayambua

Tumejipanga ili kutoa mchango bora zaidi katika vikundi vipya vya ulinzi wa amani DRC- Meja Jenerali Kapinga

Wakati Tanzania ikijiandaa kupeleka kikosi chake katika vikundi vipya vitakavyokuwa na uwezo wa kuchukua hatua haraka zaidi kukabiliana na vitisho na hatimaye kuimarisha ulinzi wa raia nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC , chini ya bendera ya Umoja wa Mataifa, mkuu wa mafunzo na utendaji wa kivita wa jeshi la wananchi wa Tanzania, JWTZ amezungumzia kile ambacho watafanya ili utendaji wao uendane zaidi na mazingira. Tupate maelezo zaidi kutoka Luteni Issa Mwakalambo Afisa habari wa kikosi cha 7 cha Tanzania kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi. FIB, cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO. 

Sauti
4'13"
Takribani saa sita mchana ya tarehe 9 Agosti 1945, bomu la nyuklia liliangushwa na Marekani kwenye mji wa Nagasaki na wingu zito lilienea mjini humo, picha hii ilipigwa  umbali wa kilometa 3 kutoka kitovu cha bomu hilo.
UN /Nagasaki International

Mkataba wa UN wa kutokomeza nyuklia kuanza kutumika Januari mwakani: Guterres asema ni hatua ya kipekee

Hatimaye mkataba wa kimataifa wa kupinga matumizi ya silaha za nyuklia, TPNW, utaanza kutumika tarehe 22 mwezi Januari mwaka ujao wa 2021 baada ya Honduras kuwa mwanachama wa 50 wa Umoja wa Mataifa kuridhia mkataba huo jana jumamosi, hatua ambayo imeelezewa kuwa zama mpya ya kutokomeza silaha za nyuklia duniani.

 

Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Kennedy Gastorn akihutubia Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo Jumanne Septemba 29, 2020
UN /Loey Felipe

Tunashukuru kwa usaidizi dhidi ya COVID-19, sasa maisha yamerejea hali ya kawaida- Tanzania

Tanzania imezungumza kwenye mjadala mkuu wa mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kuelezea msimamo wake katika masuala mbalimbali ikiwemo ushirikiano wa kimataifa, janga la ugonjwa wa Corona, COVID-19, amani na usalama maziwa makuu na mustakabali wa Umoja wa Mataifa wakati huu ambapo chombo hicho kinatimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake.

 

Sauti
2'59"
Kikundi cha utamaduni cha walinda amani kutoka Tanzania kikifanya onesho kwenye mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
TANZBATT 7/Ibrahim Mayambua

TANZBATT-7 yatumia sanaa kuimarisha amani DRC

Sanaa katika operesheni za ulinzi wa amani zinazofanywa na Umoja wa Mataifa kwenye mataifa mbalimbali ikiwemo Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC imedhihirika  kuwa mbinu muhimu ya kuleta utangamano miongoni mwa wanajamii wa taifa hilo hususan jimboni Kivu Kaskazini kwa kuwa na ujumbe maridhawa wa amani kwa rai na kusahau magumu wanayopitia  kufuatia machafuko yaliyodumu kwa miongo kadhaa.

 

Sauti
3'11"