Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mwanasaikolojia wa kujitolea Amie akifanya kikao cha ushauri nasaha moja kwa moja na Kaddy, mwanamke wa Senegal ambaye alikimbilia Gambia.
Picha: IOM/Robert Kovacs

Msaada wa kisaikolojia nchini Gambia unasaidia watu waliofurushwa - IOM

Mgogoro ulipozuka katika kijiji cha Kaddy mapema Aprili mwaka huu, alilazimika kuacha kila kitu ili kuokoa familia yake. Makala hii iliyoandikwa na Robert Kovacs, Mshauri wa IOM katika Kuripoti na Mawasiliano nchini Gambia na kutafsiriwa na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa inaeleza namna msaada wa kisaikolojia ulivyo muhimu kwa watu wanaokimbia mizozo. 

Mtoa huduma za Afya kitengo cha Mama na Mtoto katika Zahanati ya Kata ya Mkambalani Rebeca Wami akimfanyia vipimo vya ukuaji mtoto huku mama yake akishuhudia  wakati wa wiki ya unyonyeshaji.
Hamad Rashid

Wiki ya unyonyeshaji wa watoto maziwa ya mama, imetupa uzoefu - Wanajamii Tanzania

Wiki ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa watoto ambayo ilianza tarehe mosi ya mwezi huu wa Agosti na kuadhimishwa duniani kote kwa jamii kuelimishwa kuhusu umuhimu wa mama kumnyonyesha mtoto imehitimishwa jana tarehe 7. Huko mkoani Morogoro nchini Tanzania, kwa wiki nzima mashirika mbalimbali kwa kushirikiana na serikali yamekuwa yakizungumza na wanajamii ili kufahamu uelewa wao kuhusu suala hili la unyonyeshaji na pia kuwapa elimu panapohitajika.

Sauti
1'56"