Kama ilivyo kwa Nafaka, Mbolea pia inahitajika katika soko la dunia: Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo nchini Uturuki ametembelea na kukagua shughuli zinazoendelea za ukaguzi wa meli kutoka Ukraine zenye shehena ya nafaka zinazoenda kuuzwa katika soko la kimataifa na kupongeza muungano wa wakaguzi hao kutoka Ukraine , Urusi, Uturuki na Umoja wa Mataifa kwa kazi nzuri wanayofanya ambayo itasaidia dunia kuondokana na upungufu wa chakula uliosababisha bei kupanda na kuathiri zaidi nchi zinazoendelea zenye rasilimali chache kuweza kukidhi mahitaji ya wananchi wake.