Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiwa katika meli ya majaribio kupitia bahari ya Marmara nchini Uturuki ili kumtazama Kamanda Jasiri.
UN Photo/Mark Garten

Kama ilivyo kwa Nafaka, Mbolea pia inahitajika katika soko la dunia: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo nchini Uturuki ametembelea na kukagua shughuli zinazoendelea za ukaguzi wa meli kutoka Ukraine zenye shehena ya nafaka zinazoenda kuuzwa katika soko la kimataifa na kupongeza muungano wa wakaguzi hao kutoka Ukraine , Urusi, Uturuki na Umoja wa Mataifa kwa kazi nzuri wanayofanya ambayo itasaidia dunia kuondokana na upungufu wa chakula uliosababisha bei kupanda na kuathiri zaidi nchi zinazoendelea zenye rasilimali chache kuweza kukidhi mahitaji ya wananchi wake. 

Katibu Mkuu Antonio Guterres akipanda meli ya Kubrosliy huko Odesa, Ukraine.
UN Photo/Mark Garten

Kila meli inayoondoka Odesa imebeba matumaini- Guterres

Leo hii Odesa ni zaidi ya bandari ya kusafirisha, shehena, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo alipotembelea bandari hiyo iliyoko Ukraine, kujionea upakiaji wa shehena za nafaka na chakula kufuatia makubaliano ya kusafirisha nafaka kupitia Bahari Nyeusi, makubaliano yaliyowezesha kuanza kusafirishwa kwa bidhaa hizo kwenda soko la dunia licha ya uvamizi unaoendelea wa Urusi nchini Ukraine. 

Mwani wa Sargassum umeharibu baadhi ya fukwe safi zaidi za Mexico.
UNDP Mexico/Emily Mkrtichian

Mwani watumika kujenga nyumba za bei nafuu nchini Mexico

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo duniani, UNDP nchini Mexico linafadhili miradi ya maabara za wabunifu wanaopatia majawabu changamoto za kijamii zitokanazo na  matatizo yanayowazunguka. Miongoni mwa miradi hiyo ni ule wa kusafisha fukwe za bahari na uchafu unaokusanywa ukiwemo mwani aina ya Sargusssum, kutumika kutengeneza nyumba. 

Sauti
2'12"
Rahot akiwa na mjukuu wake, Hassan, kijijini ambako alihamia karibu na kituo cha lishe kinachoendeshwa na SCI na kufadhiliwa na SHF.
Sara Awad – Save the Children

Napanda milima kuhakikisha mjukuu wangu anapata tiba ya Utapiamlo

Kila siku asubuhi na mapema kukipambazuka na jua kuchomoza Rahot mwenye umri wa miaka 55 huamka na kumbeba mgongoni mjukuu wake Hassan tayari kwakuaza safari ya takriban kilometa 20 yenye vilima kwenda kituo cha kumpatia lishe mjukuu huyo ili kuokoa maisha yake kutokana na kuwa na utapiamlo mkali.