Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mfanyakazi katika uzalishaji wa chanjo ya COVID-19 nchini India
© UNICEF/ Dhiraj Singh

WHO yatangaza maboresho ya mkakati wa utoaji chanjo ya COVID19

Kutokana na kuendea kunyumbulika kwa virusi vya ugonjwa COVID-19 hii leo Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limechapisha maboresho ya mkakati wa utoaji chanjo ya COVID-19 ili kukabiliana na kuenea kwa virusi vipya ya Omicron, kuendeleza ushahidi unaopatikana kutokana na kutolewa chanjo na kuendelea kujifunza kutokana na matokeo ya programu za utoaji chanjo duniani kote. 

Mjenzi mtaalamu akijenga choo katika jamii yake katika wilaya ya Burera, Rwanda. Mjenzi huyo alipewa mafunzo na UNICEF na Shirika lisilo la kiserikali la Jumuiya ya Afya ya Familia kujenga vyoo vya usafi na salama.
UNICEF/Kanobana

UNICEF yahamasisha mabadiliko chanya katika maisha na mitazamo Kaskazini mwa Rwanda

Kupitia Mpango wa UN Moja ambapo mashirika kadhaa ya Umoja wa Mataifa hushirikiana kutekeleza miradi, huko nchini Rwanda, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linafanya kazi bega kwa bega na mashirika dada likiwemo la Mpango wa Chakula Duniani, WFP na la Chakula na Kilimo, FAO kutekeleza mradi wa Baho Neza au 'Ishi Vizuri' kwa kutumia maafisa ustawi wa jamii wenyeji wanaojitolea. 

Sauti
2'41"
Mara baada ya kutiwa saini kwa makubaliano yanahakikisha ufikiaji kamili wa kimataifa kwa bidhaa za chakula za Ukraine na chakula na mbolea kutoka Kirusi. Istanbul, Uturuki.
Picha ya UN

Makubaliano yaliyotiwa saini leo Istanbul ni nguzo ya matumaini- Guterres

Hatimaye makubaliano ya kuruhusu meli zilizojaa shehena za nafaka kutoka nchini Ukraine zipite kwenye baharí nyeusi yamefikiwa hii leo huko Instanbul Uturuki baina ya Ukraine na Urusi yakishuhudiwa na katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ambaye amesema makubaliano hayo yameleta nuru kwa ulimwengu kupata ahueni kwenye bei za mazao ya chakula katika soko la kimataifa.

Sauti
3'19"