Machafuko yaliyotokea CAR yanaweza kuwa uhalifu wa Kivita: UN
Machafuko yanayoendelea nchini Jamhuri ya Afrika ya kati -CAR yanaweza kuwa uhalifu wa kivita imeeleza taarifa iliyotolewa leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za binadamu baada ya kuwasilisha ripoti zake mbili za matukio ya kutatanisha yaliyotokea kati ya mwaka 2020 mpaka mwaka huu wa 2022 nchini humo.