Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watoto waliokimbia makazi yao nchini Sudan Kusini
© UNMISS / Eric Kanalstein

Machifu Sudan Kusini wajengewa uwezo ili wawalinde watoto

Katika kuhakikisha watoto wanaoishi kwenye maeneo ya mizozo ya kivita hawahusishwi kuingia vitani, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia watoto UNICEF wamewakutanisha pamoja zaidi ya machifu 80 wa Sudan Kusini ili kuwapatia elimu ya kukomesha na kuzuia ukiukwaji wa haki za watoto.

Sauti
3'15"
Picha ya Picasso ya Guernica ikitundikwa upya nje ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa baada ya kusafishwa na wahifadhi.
UN Photo/Mark Garten)

Mchoro wa kihistoria wa Picasso unaofahamika kama Guernica warejeshwa UN

Mchoro wa kihistoria unaofahamika kama Guernica uliofumwa vizuri kwa nyuzi katika kitambaa kikubwa ukilenga kupinga vita na matukio yake, umerejeshwa tena katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa baada ya kuondolewa takribani mwaka mmoja uliopita ili usafishwe kitaalamu chini ya familia ya mfanyabiashara na mwanasiasa wa zamani wa Marekani, Marehemu Nelson Rockeffeler.

Sauti
2'30"
Essau Musinzi, mnufaika wa mashine ya kutotolesha vifaranga vya kuku, mashine ambayo walipatiwa na FAO Tanzania.
FAO Tanzania

Yai lililouzwa kwa bei ya hasara sasa lageuka faida, shukrani mashine kutoka FAO

Baada ya kuhangaika kwa muda mrefu wakipoteza mayai na mara nyingine kuuza mayai kwa bei ya chini kutokana na kukosa uhakika wa kutotolesha mayai kwa kutumia vifaa vya kisasa, hatimaye wafugaji kuku wilayani Kibondo mkoani Kigoma nchini Tanzania sasa wameanza kuona nuru, shukrani kwa kitotoleshi vifaranga au Incubator kwa kiingereza kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO. 

Soko nchini Sudan Kusini
© UNICEF/Sebastian Rich

Vikwazo bado ndio njia japo inabidi kuangaliwa kupunguza matokeo mabaya- DiCarlo 

Naibu Katibu Mkuu wa Masuala ya Kisiasa na Amani, Rosemary A. DiCarlo, leo Februari 7 ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwamba "vikwazo vinasalia kuwa chombo muhimu cha Mkataba kilichopo kwa Baraza ili kuhakikisha udumishaji wa amani na usalama wa kimataifa, "lakini akasisitiza kuwa" mengi zaidi yanaweza kufanywa ili kupunguza matokeo mabaya yanayoweza kutokea” ya vikwazo hivi. 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, Rashidi Mchata, (kushoto) akipokea televisheni 14 na laptop 9 zilizotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo,FAO. Katikati ni Mwakilishi Msaidizi wa FAO nchini Tanzania, Charles Tulahi.
FAO Tanzania

FAO yakabidhi vifaa vya kidijitali Kigoma Tanzania

Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO hii leo limekabidhi seti 14 za televisheni na kompyuta ndogo 9 kwa serikali ya mkoa wa Kigoma nchini Tanzania ili kusaidia kusongesha uelewa wa jamii kuhusu masuala ya lishe na kutumia pia mawasiliano ya kidijitali katika kuimarisha sekta ya kilimo.