Idara ya zimamoto mjini Juba Sudan Kusini yaishukuru UNMISS kwa msaada wake wa magari
Mamlaka mjini Juba Sudan Kusini zimeushukuru Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS ambao umetoa msaada wa magari mawili makubwa ya huduma za uzimaji moto katika nchi hiyo ambayo miundombinu yake na huduma za kijamii vimeharibiwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe iliyodumu kwa takribani miaka mitano.