Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Waudumu wa WHO wakiwa kwenye shughuli katika kambi ya kanyaruchinya wilayani Nyiragongo-Goma
UN News/ Byobe Malenga.

Chanjo dhidi ya Kipindupindu yaendelea Kivu Kaskazini, DRC- WHO

Kampeni ya utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu  iliyoanza tarehe 25 mwezi huu huko Kivu Kaskazini nchini jamhuri ya Kidemokraia ya Congo, DRC imekunja jamvi jana Jumanne ya tarehe 30 mwezi hu uwa Januari ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO lilizindua kampeni hiyo ya chanjo kwa wakimbizi wa ndani katika kambi ya wakimbizi hao ya Kanyaruchinya wilayani nyiragongo katika mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini.

Sauti
5'30"
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa, Kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 katika doria ya barabara ya Mbau-Kamango
TANZBATT 9

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wafanya doria barabara inayounganisha DRC na Uganda

Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini. 

Sauti
1'45"
Wapiganaji wa M23 wakielekea Goma nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC
MONUSCO/Sylvain Liechti

Raia 18 wamejeruhiwa na 4 mahutusi katika machafuko Kivu Kaskazini DRC:UN

Taarifa kutoka mpango wa Umoja wa Mastaifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC zinasema hali katika Mashariki mwa nchi hiyo bado ni ya wasiwasi mkubwa , huku kukiwa na ripoti za mapigano kati ya wanajeshi wa serikali FRDC na kundi la wapiganaji la M23 kusini na kusini-mashariki mwa eneo la Kitchanga, katika jimbo la Kivu Kaskazini. 

Makazi mapya yaliyojengwa na UNHCR Nyiragongo kwa ajili ya wakimbizi wa ndani
UN News Video/Byobe Malenga

UNHCR yajenga makazi mapya 3,000 kusaidia wakimbizi wa ndani Nyiragongo DRC

Takriban watu 233,000, wamelazimika kuyahama makazi yao katika wilaya ya Nyiragongo jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kutokana na vita vinavyochochewa na kundi la wapiganaji waasi la M23 na zaidi ya asilimia 95% ya watu hawa wanaripotiwa kuishi katika makanisa, shule, viwanja vya michezo na wakati wengine wanaishi na familia zinazowapokea.  

Walinda amani kutoka Tanzania waanzisha kampeni ya "Afya na Amani" nchini CRC
Picha: MONUSCO

Baada ya Mavivi, walinda amani wa UN kutoka Tanzania wafikisha misaada Hospitali ya Oicha, DRC

Kikosi cha 9, TANZBATT 9 cha wanajeshi walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo DRC-MONUSCO, wameendelea na kampeni yao ya Afya na Amani ambapo hadi tarehe 13 mwezi huu wa Januari watakuwa wakiendelea kutoa misaada kwa jamii inayoishi katika eneo lao la kazi, kaskazini mashariki mwa nchi.

Sauti
2'13"