Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Watoto mkoani Kigoma wakifurahia uji uliopikwa kwa kutumia viazi lishe. (Maktaba)
FAO Tanzania

Japani, UNHCR kuwezesha Tanzania kukidhi mahitaji ya dharura kwa wakimbizi wapya kutoka DRC

Japan imelipatia shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) nchini Tanzania msaada wad ola za kimarekani 500,000 kwa ajili ya huduma za usafi na kujisafi, WASH, halikadhalika makazi salama, maji na mahitaji mengine muhimu kwa wakimbizi wapya kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo (DRC), walioingia mkoani Kigoma, magharibi mwa Tanzania. 

Meja Rhandika. Yeye ni Kiongozi la kikosi cha wanawake ndani ya INDIBAT-1.
MONUSCO

Uwepo wa wanawake kwenye INDIBAT-1 nchini DRC kwaleta matumaini kwa wanawake

Mwezi huu wa Oktoba ikiwa ni miaka 23 tangu kupitishwa kwa azimio namba 1325 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu wanawake katika harakati za amani na usalama ninakupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kusikia jinsi ujumuishaji wa wanawake walinda amani kwenye kikosi cha India kinachohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo (MONUSCO) kumeleta matumaini kwa wanawake. 

Picha hii ya mwaka 2020 ikionesha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Malawi wakati wakilinda amani kwenye eneo la Kamango jimboni Kivu Kaskazini.
UN/Michael Ali

Baraza la Usalama: tuko tayari kuamua hatima ya MONUSCO kuondoka DRC

Likijibu ombi lililotolewa na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, la kutaka kuharakishwa kwa ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo, MONUSCO, kuondoka kuanzia mwisho wa 2023, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limetangaza kuwa liko "tayari kuamua, ifikapo mwisho wa 2023, juu ya mustakabali wa MONUSCO, uondoaji wake wa kimaendeleo, uwajibikaji na uendelevu na hatua madhubuti na za kweli zinazopaswa kuchukuliwa kama kipaumbele kutekeleza uondokaji huo”.

Bw. Jean Tobie Okala, Msemaji wa MONUSCO, ofisi ya Beni-Lubero, DRC.
UN News/George Musubao

MONUSCO inafanya nini kufanikisha uchaguzi mkuu DRC?

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, (MONUSCO) unashiriki katika maandalizi ya uchaguzi mkuu nchini humo unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu ambapo tayari umeshasaidia usafirishaji wa nyaraka za uchaguzi, halikadhalika mafunzo kwa polisi wa kitaifa ili uchaguzi huo uwe huru na ufanyike kwa amani. 

Sauti
4'53"