Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Mabadiliko ya tabianchi ndio kikwazo cha Maisha bora na kutoridhika duniani: WESP
Mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi, kuendelea kwa pengo la usawa, kuongezeka kwa mzigo wa madeni na ongezeko la viwango vya kutokuwa na uhakika wa chakula na utapiamlo vinaathiri ubora wa maisha katika jamii nyingi na kuchangia hali ya kutoridhika umeonya Umoja wa Mataifa hii leo katika ripoti yake ya hali ya uchumi duniani na matarajio mwaka 2020 (WESP).
WFP yasema watu milioni 45 wanakabiliwa na janga la njaa kusini mwa Afrika
Watu milioni 45 wengi wakiwa wanawake na watoto katika mataifa 16 ya nchi zinazoendelea Kusini mwa Afrika wanakabiliwa na hali mbaya ya kutokuwa na uhakika wa chakula kufuatia kujirudia kwa hali ya ukame, kusambaa kwa mafuriko na kuyumba kwa uchumi.
Watu milioni 45 wanakabiliwa na janga la njaa kusini mwa Afrika:WFP
Watu milioni 45 wengi wakiwa wanawake na watoto katika mataifa 16 ya nchi zinazoendelea Kusini mwa Afrika wanakabiliwa na hali mbaya ya kutokuwa na uhakika wa chakula kufuatia kujirudia kwa hali ya ukame, kusambaa kwa mafuriko na kuyumba kwa uchumi.