Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mazambara, Zimbabwe, ambapo mvua imeadimika, mwanamke anaonyesha sahani ya cicagas, moja wapo ya chaguzi za chakula wakati uwiano wa chakula wa WFP utakapomalizika.
WFP/Matteo Cosorich

Mabadiliko ya tabianchi ndio kikwazo cha Maisha bora na kutoridhika duniani: WESP

Mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi, kuendelea kwa pengo la usawa, kuongezeka kwa mzigo wa madeni na ongezeko la viwango vya kutokuwa na uhakika wa chakula na utapiamlo vinaathiri ubora wa maisha katika jamii nyingi na kuchangia hali ya kutoridhika umeonya Umoja wa Mataifa hii leo katika ripoti yake ya hali ya uchumi duniani na matarajio mwaka 2020 (WESP).