Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

UNESCO/Eric Falt

WHO: Msizike marehemu wa majanga kwenye makaburi ya halaiki

Kunapotokea majanga au vita na kusababisha watu wengi kupoteza maisha kunakuwa na hofu kuhusu miili ya marehemu kuwa inaweza kusababisha mlipuko wa magonjwa hivyo baadhi ya jamii kwa kutokuwa na taarifa sahihi hujikuta wakizika miili hiyo katika makaburi ya halaiki ili kuepuka mlipuko wa magonjwa lakini shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO linasema hiyo si sahihi. 

Kuzika marehemu ni ibada, ni heshima na kubwa zaidi husaidia wafiwa kuponya nafsi zao kwa kufunga ukurasa wa mpendwa wao wakibaki na matumaini kuwa wamempumzisha katika nyumba yake ya milele. 

Sauti
3'

08 SEPTEMBA 2023

Hii leo jaridani tunaangazia habari za masikitiko kuhusu watototo katika migogoro nchini DRC. Pia tunamulika pengo katika usawa wa kijinsia.  Makala tunarejelea ufafanuzi wa ibara ya 9 ya Tamko la Umoja wa Mataifa la haki za binadamu na mashinani tunakuletea ujumbe wa vijana kuhusu mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
11'22"

07 SEPTEMBA 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Magavana Dkt. Wilber Ottichilo wa Kaunti ya Vihiga na Gavana wa Kaunti ya Narok, Patrick Ole Ntutu hivi karibuni walipohudhuria Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu SDGs lijulikanalo kama HLPF hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, waliketi na Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa ili waeleze mipango yao ya kutimiza Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu, SDGs katika majimbo yao huko nchini Kenya.

Sauti
9'58"

06 SEPTEMBA 2023

Hii leo jaridani tunaangazia Mkutano wa Afrika kuhusu tabianchi nchini Kenya leo hii ikifunga pazia. Pia tunamulika kazi za walinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR. Makala na mashinani tunasalia nchini Kenya katika mkutano wa Afrika kuhusu kukuletea ujumbe wa vijana.

Sauti
10'44"

05 SEPTEMBA 2023

Hii leo jaridani tunaangazia mada kwa kina ikimulika Siku ya kimataifa ya hisani  au kuwaonea huruma wagonjwa na maskini. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo yanayojiri katika mkutano wa Afrika kuhusu tabianchi nchini Kenya na ujumbe wa Rais wa mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Csaba Kőrösi akitamatisha awamu yake hii leo. Katika mashinani tunakupeleka nchini DRC, kulikoni?

Sauti
16'23"