15 SEPTEMBA 2022
Hii leo katika Habari za UN ni mada kwa kina na Flora Nducha anakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako Umoja wa Mataifa umewezesha vijana sasa kuweza kujihudumia kupitia mafunzo ya kutengeneza simu janja. Msichana Sintyashi Kyaula anaeleza hali ilivyokubwa kabla ya mafunzo na baada ya mafunzo, akiwa kwenye kioski chake cha kutengeneza simu kwenye kitongoji cha Majengo, Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini.