Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

16 Machi 2022

Hii leo Jaridani Leah Mushi anakuletea sehemu ya pili na ya mwisho ya mahojiano na Jaji wa Mahakama ya Rufaa nchini Kenya, Hannah Okwengu kuhusu manufaa ya jicho la jinsia kwenye mahakama na kile ambacho wamefanikiwa ikiwemo kuanzisha Mahakama ya Familia inayohusika na kesi za ukatili wa kijinsia.

Sauti
11'37"

15 Machi 2022

Hii leo jaridani Leah Mushi anamulika: Hofu na shaka inayotawala kwa familia zilizoko ukimbizini ndani ya Ukraine huku waume au baba zao wakisalia kwenye mapigano; Wito wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kwa serikali Myanmar izuie vikosi vyake vya usalama kushambulia raia; Walinda amani wanawake wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wakihudumu Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR wapaza sauti wanavyojisikia kuhudumu chini  ya bendera ya UN na mchango wao kwenye amani; Makala anabisha hodi kwenye kongamano la kimataifa la lugha ya kiswahili linaloendelea jijini Arusha nchini Tanz

Sauti
12'53"

14 Machi 2022

Hii leo jaridani Leah Mushi anakuletea Habari kwa Ufupi zikimulika ufunguzi wa mkutano wa 66 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake duniani, CSW66, hali ya chakula Yemen yazidi kudorora na siku ya Hisabati duniani na nafasi yake katika kukabili changamoto za sasa.
Kisha ni mada kwa kina ambayo Assumpta Massoi amezungumza na Jaji Hannah Okwengu wa Mahakama ya RUfaa nchini Kenya kuhusu umuhimu wa jicho la kijinsia kwenye mahakama, hususan uwepo wa majaji wanawake.

Sauti
13'12"

11 Machi 2022

Hii leo jaridani Flora Nducha anakuletea mada kwa kina inayomulika harakati za Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la chakula na kilimo FAO nchini Tanzania za kuwezesha wanawake kushiriki katika sekta ya uvuvi huko mkoani Kigoma kupitia mradi wa FISH4ACP ambako wanawake wamepaza sauti jinsi  ushiriki wao umesaidia kuinua kipato cha familia.

Sauti
11'14"

10 Machi 2022

Hii leo jaridani mwenyeji wako Flora Nducha anamulika:
1.    Ripoti ya Benki ya Dunia na UNICEF kuhusu kutwama kwa vipato kwenye familia zenye watoto kutokana na janga la COVID-19.
2.    Kunasuliwa kutoka vitani kwa watoto nchini Sudan Kusini.
3.    Huko Bangladesh mradi wa IFAD wasababisha jamii kushangaa mwanamke kuendesha gari.

Sauti
13'46"

09 Machi 2022

Hii leo jaridani Leah Mushi anakutelea Habari kwa Ufupi zikisomwa na Flora Nducha ambamo anaangazia mwongozo wa WHO wa utoaji mimba ulio salama, madhila zaidi kwa wananchi wa Syria ambako mzozo unaingia mwaka wa 12 na UNICEF yapeleka dawa kunusuru wanawake na watoto majimbo ya Beni na Yobe nchini Nigeria.

Sauti
14'29"

08 Machi 2022

Hii leo jaridani ni siku ya wanawake tukimulika ujumbe kuanzia ngazi ya Umoja wa Mataifa wa kutaka ujumuishaji wa wanawake katika ngazi zote za maendeleo ili kufanikisha ajenda 2030 ya maendeleo endlevu. Huko Uganda wakimbizi na wenyeji kwenye makazi ya wakimbizi ya Kyangwali ni shamrashamra na ujumbe mahsusi wa siku ya leo ya wanawake duniani.

Sauti
13'59"

07 Machi 2022

Leo jaridani Leah Mushi anakuletea mada kwa kina ikiangazia siku ya wanawake duniani kesho Machi 8 ambapo kutoka Tanzania Mratibu wa shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEP nchini humo anamulika umuhimu wa wanawake na mazingira katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Lakini kwanza ni habari kwa ufupi kuhusu mauaji ya walinda amani wanne wa Umoja wa Mataifa huko Mali; watoto wanaokimbia Ukraine bila wazazi na walezi na umuhimu wa kuwekeza katika sekta ya huduma na malezi kwa watoto, wazee na wagonjwa ili kuongeza ajira milioni 300 ifikapo mwaka 2035.

Sauti
10'31"

04 Februari 2022

Hii leo jaridani Leah Mushi ana mambo makuu matatu: 
1.    Muhtasari wa Habari ukimulika Ukraine hasa kupitishwa kwa azimio la kuanzisha Kamisheni ya kuchunguza madhila yatokanayo na uvamizi wa Urusi nchini Ukraine. Kuanzishwa kwa njia ya kuwezesha raia kuondoka Ukraine na hatimaye Ethiopia ambako hali huko Tigray na Amhara yatia hofu licha ya kuimarika hivi karibuni.

Sauti
12'

3 Machi 2022

Jaridani hii leo Leah Mushi anaanzia huko Ukraine ambako mashambulizi yanayoaendelea yanahatarisha afya ya uzazi ya wanawake na watoto wa kike. Kisha anamulika siku  ya kimataifa ya wanyapori akiangazia ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa kutaka kuendelea kulindwa kwa wanyamapori kwa maslahi ya binadamu na sayari duniani. Suala la uwezeshaji wanawake kiuchumi linamulikwa pia kwa kubisha hodi Kigoma nchini Tanzania ambako Umoja wa Mataifa kupitia FAO unawapa wanawake uwezo wa kujiamini kupitia kilimo cha maharage.

Sauti
13'25"