Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UN News

Tuna njaa, ni maafa, asema mkimbizi wa Syria aliyeko Lebanon. UNHCR inajitahidi kusaidia. 

Ripoti hiyo ya Benki ya Dunia na UNHCR imechunguza madhara ya ugonjwa wa COVID-19 katika kuwasukuma wakimbizi wa Syria katika umaskini, wao pamoja na wenyeji wao nchini Jordan, Lebaon na aneo la Kurd nchini Iraq.  Ahimidiwe Olotu na taarifa zaidi.

Ripoti hiyo inasema watu wanaokadiriwa kufikia milioni 4.4 katika jamii wenyeji, na pia takribani wakimbizi milioni moja wa Syria, na Wairaq wengine 180,000 waliokimbia makazi yao wameanguka chini ya mstari wa umaskini tangu mwanzo wa janga la COVID-19. 

Sauti
2'36"
UNICEF/Mauricio Bisol

UNICEF yasema hali bado ni tete kwa watoto Cabo Delgado

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema takribani watoto 250,000 wamekimbia makazi yao kutokana na ghasia zinazoendelea kwenye jimbo la Cabo Delgado kaskazini mwa Msumbiji na sasa wako hatarini kupata magonwa ya kuambukiza kwa kuwa msimu wa mvua unaanza. Jason Nyakundi na maelezo zaidi.

 Hofu kubwa ya UNICEF ni kwamba huduma za kujisafi pamoja na maji safi na salama hazitoshelezi mahitaji yanayoongezeka ya watoto na familia zao kwenye kambi zao za muda ambamo wamejaa kupindukia.

Sauti
1'54"
UNICEF/UNI179012/Alessio Romenzi

Msimu wa baridi ukianza madhila ya wakimbizi Lebanon yanaongezeka

Maelfu ya wakimbizi nchini Lebanon sasa wanaanza kuhaha kwani majira ya baridi yamewadia na kila mwaka huwapa changamoto kubwa lakini mwaka huu madhila yanatarajiwa kuongezeka kutokana na mgogoro wa kiuchumi na mfumoko wa bei ulioanza Oktoba mwaka 2019 ambao sasa umefikia asilimia 174. Yote haya yanamanisha fedha na msaada wanaopewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR hautokidhi mahitaji.

Sauti
2'26"
Muse Mohammed/IOM

Soko la wakulima sasa liko wazi baada ya kufungua wakati wa covid-19

Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa WFP wiki hii limelifungua  tena soko kubwa la wakulima kwenye kambi ya wakimbizi wa Rohingya ya Cox’s Bazar nchini Bangladesh baada ya kulifunga kwa miezi kadhaa kufuatia mlipuko wa janga la corona au COVID-19. Soko hilo ambalo ni sehemu ya mradi wa WFP ni neema sio tu kwa wakimbizi bali pia jamii inayowahifadhi.

Sauti
2'35"