UNICEF inasema, ebola imeongeza idadi ya watoto waliotenganishwa na wazazi DRC
Watoto zaidi ya 32 wamepoteza au kutenganishwa na mzazi mmoja au wote kutokana na Ebola tangu kuzuka kwa mlipuko mpya Juni Mosi kwenye jimbo la Equateur Magharibi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC,limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.
Katika taarifa iliyotolewa leo mjini Kinshasa shirika hilo limeonya kwamba hatua za haraka zinahitajika kuongezwa sasa kabla hali hiyo haijageuka kubwa janga kubwa.