Sikutaka kuolewa, nilitaka kusoma lakini ikashindikana: Bi Habiba
Kutana na Habiba alimaarufu kama “Mama Solange” binti aliyelazimika kuacha shule na kuolewa akiwa na umri mdogo nchini Cameroon
Kutana na Habiba alimaarufu kama “Mama Solange” binti aliyelazimika kuacha shule na kuolewa akiwa na umri mdogo nchini Cameroon
Wakati tulipoanzisha chama cha wandishi wa habari wanawake, TAMWA visiwani Zanzibar nchini Tanzania kulikuwa na matukio mengi ya ukatili wa wanawake ambapo vyombo vya habari wakati huo havikuripoti na mbaya zaidi mtazamo wa jamii ukimwelekezea mwanamke lawama.
Watu zaidi ya 500 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wamelazimika kusaka hifadhi katika nchi jirani ya Uganda kufuatia mapigano mapya yaliozuka juma lililopita nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.
Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, doria inayofanywa kwa ushirikiano wa jeshi la polisi la nchi hiyo, polisi wa Umoja wa Mataifa UNPOL wanaohudumu katika mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo ujulikanao kama MINUSCA inasaidia kuweka utulivu na kukabiliana na uhalifu.
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP leo limeainisha maeneo 15 ambayo yatahitaji msaada wa dharura na uwekezaji kwa mwaka huu wa 2020.
Leo tarehe pili mwaka 2020, umeshuhudiwa uzinduzi wa mkakati wa Umoja wa Mataifa wa majadiliano makubwa zaidi ya kimataifa kuhusu mstakabali wa dunia. Ni majadiliano makubwa ya pamoja kuhusu jukumu la ushirikiano wa kimataifa katika kujenga mstakabali bora kwa wote. Mpango huo utashuhudia Umoja wa Mataifa ukichochea majadiliano katika mwaka huu mpya wote wa 2020 kwenye mazingira tofauti kote duniani.