Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UNICEF/Thomas Nybo

COVID-19 imetugeuza wafungwa, sina mtandao wa kufuatilia masomo - Mtoto DRC

Watoto nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, hivi sasa licha ya kutokwenda shuleni kutokana na janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19, wanatumia muda huo kusoma nyumbani, kusaidia kazi sambamba na kuelimisha jamii ili ijikinge na virusi hivyo.  

Kutana na mtoto Cornell Mbonyi, mkazi wa Goma jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.

Hapa amempigia simu mwenzake kumsalimu na kutaka kufahamu iwapo ana taarifa zozote za lini shule itafunguliwa kwani hata yeye Cornell hafahamu chochote.

Sauti
1'48"
Sang Huachao

Udaktari ni wito na ukiwa wako huchoki:Dkt. Wambugu

 Huyo ni mmoja wa madaktari kambini Kakuma Dkt. Jesse Wambugu akisema anafanya kazi kama afisa msaidizi wa afya kwenye kambi hiyo inayohifadhi wakimbizi takribani 196,000.

Licha ya changamoto na kuhudumia wagonjwa wengi kila uchao Dkt. Wambugu nasema

“Kinachonihamasisha kwanza kabisa ni wahudumu wa afya hapa ambao wako mstari wa mbele. Wana fanyakazi usiku na mchana kuhakikisha vituo viko tayari kupokea wagonjwa wowote”

Sauti
1'50"
UNMISS\Denis

Kutoka kutumikishwa vitani Sudan Kusini hadi kumiliki karakana ya samani

 Nchini Sudan Kusini, watoto waliokuwa wametumikishwa vitani na hatimaye kuachiliwa huru sasa wameanza kubadili maisha yao na ya wengine baada ya kupatiwa stadi za kujipatia kipato kwa msaada wa Umoja wa Mataifa na wadau wake.

Miongoni mwa watoto hao ni Malis, si jina lake halisi ambaye sasa anamiliki karakana ya kutengenza samani huko Yambio  jimboni Equatoria Magharibi.

Sauti
2'35"
Picha ya UNAMID/ Hamid Abdulsalam

COVID-19 si ukomo wa masomo kwa wakimbizi

Nchini Kenya matangazo ya shule kwa njia ya redio sasa yameanza katika kambi za wakimbizi ambapo walimu wanafundisha masomo kupitia redio za jamii ili wanafunzi waendelee na masomo hata wakati huu wa kusalia nyumbani kutokana na janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.

Kambini Dadaab nchini Kenya, mwalimu Amina Hassan akiwa katika studio ya Radio Jamii ya Gargaar, tayari kufundisha wanafunzi wake wa darasa la 5 wapatao 100 somo la kiingereza.

Sauti
1'35"
WFP/Challiss McDonough

Hatma ya watoto milioni 370 iko njia panda kisa? COVID 19:UNICEF/WFP

Mustakbali wa watoto milioni 370 uko njiapanda kwa sababu ya janga la virusi vya corona au COVID-19 lililosababisha kufungwa kwa shule zilizokuwa mkombozi wa lishe yao imesema taarifa ya mashirika ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo.

Katika shule ya mfalme George wa nne wanafunzi wakionekana kuwa na furaha sio tu kwa sababu ya masomo bali pia kutokana na mlo waliokuwa wakipatiwa bure shuleni kila siku , mlo ambao sasa ni vigumu kuupata kwani shule zimefungwa kutokana na COVID-19,

Sauti
2'18"
UN Photo/Martine Perret

Nilikuwa nakufa, wahudumu wameniokoa-aliyepona COVID-19

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mmoja wa manusura wa ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 amesihi raia wa taifa hilo la Maziwa Makuu Afrika waitikie wito wa kujikinga na gonjwa hilo akisema kuwa yeye ni shuhuda aliyenusurika.

Manusura huyo Adrien Bali mwenye umri wa miaka 56 amesema haoy akizungumza kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, kwenye mji mkuu wa DRC, Kinshasa.

Sauti
2'