COVID-19 imetugeuza wafungwa, sina mtandao wa kufuatilia masomo - Mtoto DRC
Watoto nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, hivi sasa licha ya kutokwenda shuleni kutokana na janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19, wanatumia muda huo kusoma nyumbani, kusaidia kazi sambamba na kuelimisha jamii ili ijikinge na virusi hivyo.
Kutana na mtoto Cornell Mbonyi, mkazi wa Goma jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
Hapa amempigia simu mwenzake kumsalimu na kutaka kufahamu iwapo ana taarifa zozote za lini shule itafunguliwa kwani hata yeye Cornell hafahamu chochote.