Watendaji wa UM wawasili Aleppo, uhamishaji raia warejea
Kazi ya kuondoa raia kutoka Aleppo nchini Syria ambako mapigano yameshika kasi, imeanza tena baada ya kusitishwa kwa zaidi ya siku moja huku watendaji 20 wa Umoja wa Mataifa wakiwasili eneo hilo kuhakikisha uhamaji wao unakuwa salama.
Hatua hiyo imekuja baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupitisha azimio siku ya Jumatatu lililoridhia kupelekwa kwa watendaji hao wa Umoja wa Mataifa.