Ban atuma salamu za rambirambi kufuatia shambulio la ugaidi Ujerumani
Pakua
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ametuma salamu za rambirambi kufutia vifo vya watu 12 baada ya shambuliolinalodaiwa kuwa la kigaidi mjini Berlin Ujerumani
Polisi mjini humo wanasema ajali ya lori lililoacha njia na kuvamia soko maarufu kwa maandalizi ya krisimasi ilikuwa ya makusudi .
Taarifa ya msemaji wa Ban, imemnukuu Katibu Mkuu akizipa pole familia zilizopoteza wapendwa wao katika tukio hilo, serikali na watu wa Ujerumani pamoja na kuwatakia majeruhi uponyaji.
Amesema ana amatumaini kuwa yeyote aliyehusika katika kupanga ajali hiyo atafikishwa katika mkono wa sheria haraka.