Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Rosie Paul (kushoto) na Sridevi Changali walianzisha Studio ya Masons Ink mnamo 2013
© Grace Barrett

Wanawake tunaweza tumedhihirisha katika usanifu majengo India: Rosie na Sridevi

Wakati jukwaa la kamisheni ya hali ya wanawake duniani kikao cha 68 au CSW68 likiendelea hapa makao Makuu ya Umoja wa Mataifa likibeba maudhui yanayochagiza usawa wa kijinsia na kuwezesha wanawake leo tunakukutanisha na wanawake wa shoka, maswahiba wawili wahandisi wa usanifu majengo waliodhamiria kujenga mnepo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na kupunguza changamoto ya hewa uka katika sekta ya ujenzi kwa kutumia tofali za matope. 

Mamilioni ya watu kote ulimwenguni wanapoanza kuadhimisha mwezi Mtukufu wa Ramadhani, kwa huzuni huko Gaza na katika eneo lote, wengi wataadhimisha mwezi huu wakikabiliwa na migogoro, kufukuzwa na hofu.
© UNRWA

Ni wakati wa Ramadhan tusitishe uhasama Gaza na Sudan: Guterres

Leo ni mwanzo wa mwezi mktukufu wa Ramadhan ambapo Waislamu kote duniani hudumisha na kuchagiza tunu za amani, maridhiano na mshikamano lakini uhasama unaendelea hususani sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Gaza ambako mauaji , na mashambulizi hayajakoma amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza na waandishi wa habari mjini New York Marekani hii leo. 

Sauti
2'53"